24 May 2015

Jinsi ya kujiunga na mifumo ya PayPal na Moneybookers.


Ndio, kabla hatujaangalia namna ya kujiunga na paypal au moneybookers, hebu na tuangalie pros and cons (faida na hasara) za kutumia kadi yako kwwnye manunuzi mtandaoni, na kwamba paypal au moneybookers ni mkombozi wako.

·         Kwanza tambua kuwa, mtu akizifahamu namba za kadi yako anaweza kuchukua pesa zote kwenye akaunti bila ridhaa yako. Kwa kadi za visa hata mastercard kuna namba namba zimepangwa nne kwenye mafungu manne na zinaunda idadi ya tarakimu 16 (zinaitwa credit card number) na pia zinafuatiwa na namba zingine tatu upande wa nyuma wa kadi (zinaitwa card veeification code). Hizi namba ni mhimu kuzificha kila unapofanya shughuli yoyote kuhusiana na hiyo kadi yako.

·         Pili, utakwepa vipi maana ili ununue ni lazima utaingiza hizo namba zote kwenye mfumo ule unaotumika kununua bidhaa au huduma, utakwepaje sasa? Haupo salama sana kwani endapo muuzaji akiamua kukurudia atakuchukulia pesa maana tayari umeshampa details mhimu za kadi yako.

PayPal

Huu ni mfumo unaomilikiwa na soko la ebay, ni mfumo uliotapakaa karibu kila soko la bidhaa au huduma mtandaoni. Taratibu za kujiunga ni kwenda kwenye tovuti yao www.paypal.com ambapo utajisajili na kupata akaunti. Kawaida yao watakata pesa kiasi cha dola moja na nusu kwa wakati huu naandika wanakata hivyo, kama utasoma maelezo haya wakati ambao imebadilika tafadhali usinihukumu. wanafanya hivyo ili kuhakiki akaunti yako na watairudisha ndani ya siku thelathini. Baada ya kukukata hicho kiwango cha pesa, watakutumia tarakimu nne kwenye statement ya akaunti yako. Ila usije ukasumbuka kwenda benki kuomba statement ukitegemea utauona huo muamala na hizo tarakimu kwenye statement yako, ni kwamba hautauona. Unaweza kuziona tu kwa njia ya internet kwa wale waliojiunga na ebanking.
Baada ua kuukamilisha huo mchakato sasa uko tayari kufanya malipo kwa njia salama kwani paypal hawatahitaji uweke namba za kadi yako kila unapotaka kununua na hawatatoa hizo namba kwa muuzaji.

Moneybookers

Taratibu za kujiunga na moneybookers zinafanan na zile za paypal. Ingia kwenye tovuti yao www.moneybookers.com na ujiunge. Tofauti na paypal ambao hukata kiwangi cha pesa na kukutumia tarakimu nne, monebookers wao huchukua kiwango cha pesa na kukuuliza utaje umekatwa kiasi gani kutoka kwenye akaunti yako. Ki msingi wanataka wahakikia kama kweli akaunti ni ya kwako maana kama sio yako hautajua kiwango gani kimekatwa.

Sasa hapa ndio utaona umuhimu wa kuwa na akaunti ya dola kwani kama unatumia akaunti ya shilingi hautajua ni dola ngapi zimekatwa hata kama utajua dola imeuzwa bei gani siku hiyo. Kwa hiyo ni muhimu kufungua akaunti ya dola na pia kujiunga na internet banking ili kukwemba usumbufu mwingine usio wa lazima. Lakini usiogope unaweza ukaachana na monebookers na ukabaki na paypal sio mbaya. Kwanza paypal ndio inatumika sana kuliko moneybookers.


Hadi hapo naamini tayari umeshangua akaunti paypal na/au monebookers, nakupongeza. Sasa upo salama unapokuwa ukifanya manunuzi yako mtandaoni. Sio kazi ngumu sana japo wengine inawapa shida, ukishindwa basi tupe kazi tukufanyie. Ingia kwenye ukurasawetu wa nyumbani  na ujaze fomu ya oda nasi tutaipata na tutakuhudumia.

No comments:

Post a Comment

Tafadhali toa mchango au maoni yako hapa