Ndio,
kabla hatujaangalia namna ya kujiunga na paypal au moneybookers, hebu na
tuangalie pros and cons (faida na hasara) za kutumia kadi yako kwwnye manunuzi
mtandaoni, na kwamba paypal au moneybookers ni mkombozi wako.
·
Kwanza
tambua kuwa, mtu akizifahamu namba za kadi yako anaweza kuchukua pesa zote
kwenye akaunti bila ridhaa yako. Kwa kadi za visa hata mastercard kuna namba
namba zimepangwa nne kwenye mafungu manne na zinaunda idadi ya tarakimu 16
(zinaitwa credit card number) na pia zinafuatiwa na namba zingine tatu upande
wa nyuma wa kadi (zinaitwa card veeification code). Hizi namba ni mhimu
kuzificha kila unapofanya shughuli yoyote kuhusiana na hiyo kadi yako.
·
Pili,
utakwepa vipi maana ili ununue ni lazima utaingiza hizo namba zote kwenye mfumo
ule unaotumika kununua bidhaa au huduma, utakwepaje sasa? Haupo salama sana
kwani endapo muuzaji akiamua kukurudia atakuchukulia pesa maana tayari
umeshampa details mhimu za kadi yako.
PayPal
Huu
ni mfumo unaomilikiwa na soko la ebay, ni mfumo uliotapakaa karibu kila soko la
bidhaa au huduma mtandaoni. Taratibu za kujiunga ni kwenda kwenye tovuti yao
www.paypal.com ambapo utajisajili na kupata akaunti. Kawaida yao watakata pesa
kiasi cha dola moja na nusu kwa wakati huu naandika wanakata hivyo, kama
utasoma maelezo haya wakati ambao imebadilika tafadhali usinihukumu. wanafanya
hivyo ili kuhakiki akaunti yako na watairudisha ndani ya siku thelathini. Baada
ya kukukata hicho kiwango cha pesa, watakutumia tarakimu nne kwenye statement
ya akaunti yako. Ila usije ukasumbuka kwenda benki kuomba statement ukitegemea
utauona huo muamala na hizo tarakimu kwenye statement yako, ni kwamba
hautauona. Unaweza kuziona tu kwa njia ya internet kwa wale waliojiunga na
ebanking.
Baada
ua kuukamilisha huo mchakato sasa uko tayari kufanya malipo kwa njia salama
kwani paypal hawatahitaji uweke namba za kadi yako kila unapotaka kununua na
hawatatoa hizo namba kwa muuzaji.
Moneybookers
Taratibu
za kujiunga na moneybookers zinafanan na zile za paypal. Ingia kwenye tovuti
yao www.moneybookers.com na ujiunge. Tofauti na paypal ambao hukata kiwangi cha
pesa na kukutumia tarakimu nne, monebookers wao huchukua kiwango cha pesa na
kukuuliza utaje umekatwa kiasi gani kutoka kwenye akaunti yako. Ki msingi wanataka
wahakikia kama kweli akaunti ni ya kwako maana kama sio yako hautajua kiwango
gani kimekatwa.
Sasa
hapa ndio utaona umuhimu wa kuwa na akaunti ya dola kwani kama unatumia akaunti
ya shilingi hautajua ni dola ngapi zimekatwa hata kama utajua dola imeuzwa bei
gani siku hiyo. Kwa hiyo ni muhimu kufungua akaunti ya dola na pia kujiunga na
internet banking ili kukwemba usumbufu mwingine usio wa lazima. Lakini usiogope
unaweza ukaachana na monebookers na ukabaki na paypal sio mbaya. Kwanza paypal
ndio inatumika sana kuliko moneybookers.
Hadi
hapo naamini tayari umeshangua akaunti paypal na/au monebookers, nakupongeza.
Sasa upo salama unapokuwa ukifanya manunuzi yako mtandaoni. Sio kazi ngumu sana
japo wengine inawapa shida, ukishindwa basi tupe kazi tukufanyie. Ingia kwenye ukurasawetu wa nyumbani na ujaze fomu ya oda nasi tutaipata na tutakuhudumia.
No comments:
Post a Comment
Tafadhali toa mchango au maoni yako hapa