24 May 2015

Elimu ya manunuzi kwenye mtandao: Anza sasa



Ki msingi sio jambo la kuamka tu siku moja ukaanza kununua kwenye mtandao, ni lazima upitie hatua kadhaa kabla ya kuanza rasmi kununua kwenye mtandao. Jambo la kwanza, fungua akaunti katika benki yoyote yenye huduma za kimataifa kama vile CRDB, NBC, EXIM BANK nk ambazo zina huduma za master card na visa. Kwa NMB hadi niandikavyo maelezo haya ni kwamba hawana huduma za mastercard na/au visa. Ukishafungua akaunti hakikisha unapewa ile kadi ya ATM (credit/debit card), mara nyingi benki zetu Tanzania hutoa debit cards.

Sasa baada ya kuwa umeshafungua akaunti kwenye bank yoyete kisha ukapata kadi ya atm yenye nembo ya mastercard na / au visa, kinachofuata rudi bank uwaombe ili waiwwzeshe akaunti yako kufanya malipo kwwnye mtandao (online purchaising). Bank watakupa fomu maalumu utaijaza kisha ujikomiti kwa lolote litakalotokea katika shughuli yako ya kulipa kwenye mtandao, utaweka sahihi yako kisha wakabidhi hiyo fomu na utaambiwa kusubiri kwa muda usiopungua siku tatu (wakati mwingine unawwza kusubiri hadi mwezi mzima kutegemea na uharaka wa benki husika).

Kuna watu wengi waliwahi kuniuliza ni bank gani inafaa kuitumia kama debit card issuer kwenye manunuzi mtandaoni. Jibu sio rahisi kupatikana maana sijawahi kutumia banki zote, hata hivyo mimi ni mteja wa CRDB na ninazo sababu za kupenda kutumia CRDB. Hebu angalia mfano Standard Chartered au Exim Bank, hutakiwi kufungua akaunti kule kama wewe ni mtanzania mwenye kipato cha chini au kawaida. Huduma zao ni ghali sana na hakuna huduma ya bure. Wakati huu naandika maelezo haya, Standard Chartered wanatoza dola kumi kila mwezi kutoka kwenye akaunti yako pamoja na asilimia zingine zaidi kila unapotumia huduma zao. Kwa CRDB hayo malipo hayapo, hukatwi hela hizo. Mimi sio afisa wa CRDB ila ni mteja na ninaongea na jamii yenye utambuzi na uhuru wa kuchagua huduma toka benki yoyote.

Baada ya kuwezeshwa kadi yako sasa unastahili pongezi maana unaweza kununua unachotaka kutoka mtandaoni na kwa muda wowote hata kama umelala kitandani. Lakini pia sio kulipa tu bali hata kulipwa au kupokea malipo kwa njia hiyo ya kadi yako (Jinsi ya kupokea malipo kwa paypal na moneybookers). Lakini pia lazima ukumbuke kuwa kuna mitandao mingine sio salama kufanya malipo kwa kadi yako, unaweza ukalipa ukajikuta pesa yote haimo kwenye akauntu na utalia. Hivyo imekupasa kuchukua tahadhali kubwa na kuangalia mitandao unayotumia kununua au kulipa. Na ili uwe salama na pesa yako kwa asilimia nyingi, zipo njia na mifumo salama unayopaswa uitumie kwa usalama wa pesa zako.

Ushauri wangu, jiunge na ebanking, mimi ni mteja wa CRDB hivyo sijui benki zingine wanaitaje hiyi huduma. Ukishajiunga na ebanking utaweza kupokea, kutoa au kutumia pesa kwenye akaunti yako kwa njia ya mtandao kwa kutumia komputa au simu yako kama imeunganishwa naaa internet. Hadi naandika maelezo haya ni kwamba CRDB wanatoza elfu 30 kwa huduma hiyo na hakuna malipo ya kila mwezi au kila mwaka, hii ni mhimu sana kwa wewe unaeanza biashara kwa kutumia mtandao wa internet.

Ukishajiunga na CRDB Internet Banking, nakushauri pia fungua akaunti ya dola. Namna ya kufungua wala sio vigumu na hauhitaji kuwaza juu ya hili. Kama unayo akaunti ya CRDB basi unachotakiwa ni kuandika barua kwenda CRDB ukiomba kufungua akaunti ya dola na hautahitaji kiambatanisho kwani viambatanisho vile vile ulivyovitumia wakati unafungua akaunti ya shilingi vitatumika hivyo hivyo. Ni mhimu sana kwako wewe unayeanza biashara kutumia internet kufungua akaunti hii ya dola kwani thamani ya shilingi yetu huporomoka kila wakati. Kwa hiyo kama una dola, thamani ya shilingi ikiahuka basi wewe ya kwako imepanda.

Kuna rafiki yangu mmoja aliwahi kuniuliza akaunti ya dola inaonekanaje namba zake? Jibu ni kuwa siwezi kujua benki zingine namba zinasomekaje ila kwa CRDB ninafahamu. Mfano kama akaunti yako ya shilingi inasomeka hivi 01j20xxxxxxxx basi akaunti yako ya dola itasomeka hivi 02j20xxxxxxxx, umeona? Kinachofanyika ni kubadilika namba moja tu.


No comments:

Post a Comment

Tafadhali toa mchango au maoni yako hapa